Sept 21, 2016 majina ya mwanzo ya wasanii watakaowania tuzo za MTV MAMA
2016 yalitajwa huku Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz na kundi la Navy
Kenzo pamoja na Alikiba ndio wasanii wa Tanzania waliotajwa kuwania
tuzo kubwa za Africa za MTV Africa Music Awards 2016.
Sasa basi habari njema leo October 2, 2016 MTV MAMA 2016 wametaja majina
mengine ya wasanii watakaowania tuzo hizo ambapo kwa upande wa Tanzania
wameongezeka wasanii watatu akiwemo Raymond wa WCB, Vanessa Mdee na
Yamoto Band.
Diamond Platnumz ametajwa kwa mara ya pili kuwania tuzo hizo katika
kipengele cha Artist of the Year ambacho anachuana na Black Coffee
(South Africa), Sauti Sol (Kenya), Yemi Alade (Nigeria), Wizkid
(Nigeria).
Mara ya kwanza Diamond Platnumz alitajwa kuwania kipengele cha Best Male
ambacho anachuana na Black Coffee (South Africa), Wizkid (Nigeria), AKA
(South Africa), Patoranking (Nigeria).
Vanessa Mdee anawania kipengele kimoja cha Best Female ambacho anachuana
na Josey (Ivory Coast), Mz Vee (Ghana), Tiwa Savage (Nigeria), Yemi
Alade (Nigeria).
Alikiba ametajwa kwa mara ya pili kuwania kipengele cha Song of the Year
kupitia wimbo aliyoshirikishwa na Sauti Sol uitwao Unconditionally Bae.
Kenya imewakilishwa na kundi la Sauti Sol katika kipengele cha Song of
the year na Artist of the year pamoja na Kansoul kwenye kipengele cha
Listerners Choice Awards.
Huku Uganda ikiwa imewakilishwa na wasanii wawili ambao ni Eddy Kenzo
anayewania kipengele cha Best Live Act pamoja na Sheeba anayewania
kipengele cha Video of the Year pamoja na Bebe Cool katika kipengele cha
Listener’s Choice Awards.
Raymond wa WCB ametajwa kuwania kipengele cha Best Breakthrough Act
ambacho anachuana na Babes Wodumo (South Africa), Emtee (South Africa),
Falz (Nigeria), Franko (Cameroon), Nasty C (South Africa), Nathi (South
Africa), Simi (Nigeria), Tekno (Nigeria), Ycee (Nigeria).
Yamoto Band wametajwa kuwania kipengele cha Listener’s Choice Awards
ambacho wanachuana na Burna Boy (Nigeria), Adiouza (Senegal), Kansoul
(Kenya), Meddy (Rwanda), Prince Kaybee (South Africa), Zaho (Algeria),
Kiss Daniel (Nigeria), E.L (Ghana), Bebe Cool (Uganda), Latifa
(Tunisia), Saad Lamjarred (Morocco), Tamer Hosny (Egypt), Jay Rox
(Zambia), The Dogg (Namibia), Sidiki Diabate (Mali), Adiouza (Senegal),
Den G (Liberia), Jah Prayzah (Zimbabwe), LIJ Michael (Ethiopia), Messias
Maroca (Mozambique).
Hivi ndio vipengele 7 vipya vya wasanii watakaowania tuzo za MTV MAMA
2016, Jumamosi ya 22 October 2016 kwenye ukumbi wa Ticketpro Dome Afrika
Kusini.
Home
»
Burudani
» MTV MAMA Awards 2016..Wameongezeka Watanzania Watatu Kwenye List ya Kuwania Tuzo Hizo
Monday, October 3, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment