Jana Nasibu Abdul maarufu Diamond Platnumz alipost picha ya Wema
Sepetu katika ukurasa wake wa Instagram akiwataka watu wajitokeze
kumsupport katika tamasha. Pamoja na Wema Sepetu, Diamond alimpost pia
Idris Sultan na Christian Bella.
Diamond Platnumz aliandika hivi “Make sure ya’ all go Support Christian Bella X Wema Sepetu X Idris Sultan na wengine wakali kibao katika Usiku wa #BlackTie pale King Solomon Hall tareh 9 / 07 /2016!!! It’s all about Black and Everything!”
Hii hapa ndiyo picha iliyowekwa kwenye ukurasa wa Diamond Platnumz
Wema Sepetu alipohojiwa kuhusu kitendo hicho alisema kuwa amefurahi
sana na kuona kama kuna mzigo alioutua kwani watu walikuwa wakitumia
tofauti zao za kutengenezwa kama faida kwao ili kupata wafuasi
(Followers).
Aidha, ameeleza kuwa yeye ni shabiki wa Diamond Platnumz na amekuwa
akisikiliza nyimbo zake hata baada ya wao kuachana. Amesema kuachana
kwao hakumfanyi asiwe shabiki wake.
Alieleza kuwa kwa muda sasa amekuwa akijizuia kuimba nyimbo za
Diamond akiwa kwenye public lakini ameona kuwa anajikomoa yeye mwenyewe
kwani akirudi kwenye gari lake huwa anaimba. Kwake amesema kuwa kitendo
hicho kinaondoa uongo uliokuwa unasemwa kwamba wawili hao wana bifu
zito.
Home
»
Udaku
» #BURUDANI>>>>>Baada ya Diamond kumpost Wema Sepetu Instagram, Wema afunguka juu ya hilo.Fahamu zaidi hapa.
Thursday, July 7, 2016
Newer Post
Previous
This is the last post.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment