Huo ndio ukweli wenyewe.
Tafakari juu ya taarifa ya Benki Kuu inayoonyeha kwamba tangu Magufuli
kuingia madarakani kasi ya kukua kwa uchumi wa Taifa imepungua kwa
asilimia 4.
Tukiwa na ukuzi wa
asilimia karibu 9 kwa mwaka, Tanzania ilikuwa moja ya nchi kinara
duniani kwa kukua uchumi. Sasa suala la kujiuliza ni kwamba, kubanwa kwa
ufisadi kunakofanywa na Rais Magufuli, ni kubaya kwa kuwa kunasababisha
kasi ya uchumi wetu kupungua?
Ukweli ni kwamba ufisadi
unaongeza mzunguko wa fedha nchi, kwa kuwa mafisadi hutumia fedha kwa
wingi na hivyo kuwa kichocheo cha shughuli za kiuchumi. Matokeo yake
wafanya biashara ndogo na kubwa wote wanafaidika na fedha za ufisadi, na
kufaidika huku kunaleta kukuka kwa kiwango cha maisha (standard of
living) kwa wengi, maana watu wanakuwa wamejaa mapesa. Fedha za ufisadi
pia huingia kaitka uwekezaji na hata kutengeneza ajira katika sekta za
ujenzi, usafiri, kilimo, nk.
Kimsingi, ufisadi ni
sawa na serikali kutoa fedha kwa "taasisi" (stimulus packages) ili
kuinua kuchochea shughuli za kiuchimi, kama tu Obama alivyotoa fedha kwa
taasisi za Marekani pale hali ao ya uchumi ilipokuwa mbaya sana
wakielekea hali ya recession.
Labda kibaya ni kwamba
ufisadi unaleta mporomoko wa thamani ya fedha unaotokana na fedha nyingi
kuwa mikononi mwa wananchi (inflation). Lakini hili lilipingwa sana na
Waziri Mkuu wa zamani wa Ethiopia, Zenawi, pale ambapo serikali yake
ilitoa pesa kwa wananchi ili waanzishe miradi kama ya mahoteli ya
kitalii na majengo ya ofisi, na uchumi wa Ethiopia ukawa unakua kwa kasi
sana huku inflation rate ikipanda hadi asilimia 17. Zenawi alisema
kwamba hakuona tatizo uchumi wa nchi kukua sambamba na inflation rate.
Sasa, kuzuia ufisadi ni
kubaya? Jibu ni hapana, ila sasa, ukiwa Raisi ukabana sana ufisadi kiasi
cha kupunguza mzunguko wa fedha nchini, inabidi uangalie mianya ya
kuongeza mzunguko wa fedha, mbadala wa ufisaidi. Kwa mfano, kosa
linalofanywa na serikali ni kubana ufisadi na bado kuweka kodi nyingi
ambazo zinabana watu kufanya biashara. Angalia jinsi bandari
ilivyokauka, hatua iliyochukuliwa sambamba na kubana ufisadi. Ufisadi wa
kuingiza bidhaa kwa kukwepa kodi mara nyingi ni matokeo ya kuwapo mfumo
unaoumiza wa utozaji ushuru na kodi kwa bidhaa toka nje ya nchi.
Kwa hiyo basi, Raisi
Magufuli anapaswa kuangalia upya suala zima la utozaji kodi nchini, kwa
kuwa amebana ufisaidi. Kodi zinatakiwa zilegezwe mno, katika principle
ya "economies of scale". Kwa mfano, ule mfumo wa kukadiria na kutoza
kodi kabla hata biashara haijaota miguu inapaswa ubadilishwe. Pia kodi
na hata ushuru wa bidhaa toka nje zinatakiwa zishushwe ili kuwapa hata
wale wenye mtaji mdogo nafasi ya kuagza bidhaa za kiuwekezaji. Biashara
ndogo ndogo ambazo hazizidi mtaji wa kama milioni kumi zinaweza
kusamehewa kodi kabisa. Na pia kuwe na mfumo tofauti wa kodi kulingana
na wapi muwekezaji anawekeza; kama ni jiji, mkoa, wilaya au kijijini.
Unaweza hata kusema ukijenga kiwanda kijijini basi kodi yako inapata
punguzio la asilimia 50, tofauti na kama ukikijenga kwenye jiji.
Kwa hiyo serikali ya
Raisi Magufuli inapaswa kuchukua haraka hatua za kurekebisha mfumo wa
kodi hasa kwa kuwa mianya ya ufisadi imezibwa. Kumbuka kwamba ufisadi ni
sawa na kumbebesha mtu ndoo ya maji inayovuja. Kuvuja kwake ni nafuu ya
mchukuzi, lakini ukiziba kuvuja bila kumpa ahueni ya kupumzika kwa
namna fulani, utakuwa unamwumiza badala ya kumsaidia.
Monday, September 12, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment