Licha ya kupoteza mchezo wa jana dhidi ya Nigeria, Taifa Stars wamevuna
kitita cha dola 10,000 kutoka kwa Gavana wa jimbo la Akwa Ibom State,
Udom ambapo ndipo unapopatikana Uwanja wa Uyo uliotumika kwenye mchezo
wa jana.
Kitita hicho ni sawa na shilingi za Kitanzania ml 21.7 na Gavana huyo
alitoa wakati waliokuwa wakipata chakula cha usiku kwa pamoja baada ya
mchezo huo.
Ikumbukwe kuwa katika historia ya timu hizi mbili, Tanzania haijawahi
kuifunga Nigeria katika michezo yote waliyowahi kukutana zaidi ya
kuambulia vichapo na sare.
Gavana huyo ametoa kiasi hicho cha fedha kutokana na ari ya upiganaji
iliyooneshwa na wachezaji wa Stars, ambao walikuwa wakiongozwa na
nahodha wao Mbwana Samatta ambaye kabla ya mchezo huo alikuwa gumzo kwa
Wanigeria.
Hata hivyo, jana kuna wachezaji ambao walionesha kiwango kikubwa sana
kilichowapa mashaka Nigeria. Wachezaji hao ni pamoja na Aishi Manula,
Simon Msuva na mabeki wa kati Vincent Andew na David Mwantika.
Vilevile Gavana huyo pia aliwapa Nigeria Naira mil 10 kama pongezi kwa
ushindi wao waliopata na kuahidi kuwapa zaidi endapo watafanikiwa kupata
nafasi ya kushiriki fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Russia.
Sunday, September 4, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment