Peter Msechu amefunguka juu ya tuhuma za msanii mwenzake AT aliyedai kumzungumzia juu ya wembamba wake.
Amedai kuwa kwa mtazamo wake hajui nani amemlisha sumu msanii mwenzake
huyo lakini ameona ujumbe huo unaodai kuwa anapofanya interview amekuwa
akimzungumzia kitu ambacho ni uongo.
“Mara nyingi napofanya interview nimekuwa nikiulizwa kuhusu unene wangu
lakini nitakapotolea mfano wa mtu yeyote ambaye ni mwembamba kwenye
muziki si mbaya,” ameiambia Bongo5.
“Kuna kipindi nilikutana naye tukafanya interview pamoja na tukataniana
lakini nafikiri yeye alichukia binafsi tu lakini nafikiria ilikuwa ni
namna ya kutafuta atention tu,” ameongeza.
Hata hivyo Peter Msechu amedai kuwa hajawahi kumtaja AT kwenye interview
yake yoyote na wala hajawahi kuwa na urafiki na msanii huyo.
Friday, August 19, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment