Sunday, August 28, 2016

12:38 AM
Yule Mwana Dar es Salaam, Kingkiba, Balozi wa wanyama, Msanii pekee aliyetoboa Kimataifa bila Collabo, Kiboko ya Wizkid, Fundi na Master wa game ya mziki wa Africa "Alikiba" ambaye kwa sasa ndiyo msanii anayeongoza Kulipwa fedha nyingi kwenye Show kuliko msanii yeyote Yule East Africa.

Mwezi September kwenda kushusha Laana 5 takatifu kupitia nyimbo mpya atakazoenda kuachia 2 zake binafsi na 3 alizoshirikishwa na wasanii wa ndani na nje ya nchi,

Wajuzi na watafiti wa duru za Burudani Africa Mashariki, Wanabashiri kuwa huenda ikawa ndiyo mwanzo na mwisho wa kufunga rasmi nyufa za mziki wa bongoflava ambazo zimekuwepo kwa miaka mingi, Ambapo kwa sasa wasanii wengi wamevamia game na kukop mziki wa Nigeria bila kuzingatia misingi ya mziki wetu wa asili, Mbaya zaidi na wengine kufika mbali kutumia kiki za kihafidhina na kununua tuzo ili kupush mziki wao unaosuasua.

Note:
Kila atakayesikia project hizo mpya za KingKiba, Hakuna hata mmoja atakayethubutu kumaliza luku yake kusikiliza nyimbo zenye unaijeria, kiki na promo za kipuuzi.

0 comments:

Post a Comment