Diamond amesema kuwa hategemei muziki kuendesha maisha yake.
Hit maker huyo wa wimbo wa ‘Kidogo’ hivi karibuni kupitia kipindi maalum
cha kituo cha runinga cha E!TV, E Vip aliutaja utajiri wake kuwa ni
dola milioni 4 za Kimarekani ambao kwa shilingi ya Tanzania ni zaidi ya
shilingi bilioni 8.6.
Kupitia kipindi cha SupaMix cha EA Radio, Diamond alisema, “Ukiachilia
mbali kazi ya muziki mimi pia nina vikorokoro kibao ambavyo
vinaniwezesha kuweza kupata kipato cha kila siku.”
“Siyo kwamba muziki ni kila kitu lazima kujishughulisha na Mungu anasaidia kuweza kusonga mbele,” ameongeza staa huyo.
Tuesday, August 9, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment