Tuesday, August 9, 2016

12:27 AM
Msanii Madee leo ameweka wazi mkanganyiko ambao wengi walikuwa nao kuhusu msanii anayemsimamia Dogo Janja, mbaye pia yuko chini ya Tip Top ambayo inamsimamia yeye Madee.

Akiongea kwenye Planet Bongo ya East Africa Radio, Madee amesema ingawa Dogo Janja yupo chini yake, lakini iwapo kuna kazi anatakiwa kuifanya, lazima afanye mawasiliano na Babu Tale, na kufikia uamuzi kwa pamoja, tofauti na wengi wakivyofikiri kuwa yeye ndio ana uamuzi na Dogo Janja.

“Mtu akitaka collabo na Dogo Janja tunawasiliana na Babu Tale, na kama ishu ya kazi hawezi kukataa, lakini lazima tujadili, kwetu hatuishi kibosi bosi, kama ni jambo la msingi linawekwa mezani kila mtu anatoa maoni yake, kama afanye au asifanye”, alisema Madee.

Madee ambaye pia alianza kwa kumtoa msanii Raymond mpaka akachukuliwa na wasafi ambako yuko sasa, amesema anajivunia mafanikio ya msanii huyo, kwani tayari yupo kwenye historia yake.

0 comments:

Post a Comment