Friday, August 12, 2016

10:08 PM

Najua inawezekana wewe ni mmoja kati ya mashabiki wa soka duniani wanaosubiri kumuona staa wa kimataifa wa Ufaransa aliyejiunga na Man United akitokea Juventus ya Italia Paul Pogba akiichezea Man United katika mchezo wa ufunguzi wa Man United dhidi ya Bournemouth weekend hii.

Stori kutoka chama cha soka cha England FA kimethibitisha staa huyo kufungiwa kucheza mechi ya ufunguzi kutokana na kuwa na adhabu ya kadi mbili za njano alizooneshwa katika michuano ya Copa Italia akiwa na Juventus ya Italia, adhabu ambayo kwa mujibu wa kanuni anahama nayo.


Paul Pogba alijiunga na Man United akitokea Juventus ya Italia kwa ada ya uhamisho wa rekodi ya dunia wa pound milioni zaidi ya 100, lakini Paul Pogba anaungana na Robert Huth, Moussa Dembele na Chris Smalling  waliofungiwa na FA kucheza mechi za ufunguzi

0 comments:

Post a Comment