Na Dac Popos.
Michuano
ya Kimataifa ya Kirafiki (ICC) imeendelea kutimua vumbi kwenye viwanja
tofauti, Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza Leicester City walikiona cha
mtema kuni baada ya kuchabangwa mabao 4-2 na mabingwa wa Hispania,
Barcelona. Iliwachukuwa dakika 25 kwa washindi kuweza kuandika bao la
kwanza kupitia kwa kinda wake Munir akiunganisha pasi maridhawa kutoka
kwa Messi.
Dakika
8 baadaye yaani dakika ya 33 Suarez akaipatia Barcelona bao la pili
kutokana na mpira aliopelekewa na Messi, twaweza sema Lionel Messi
ingawa hakufunga bao lolote lakini alikuwa chachu ya ushindi kwa timu
yake kwa jinsi alivyokuwa akiiunganisha timu na kutoa pasi nyingi za
mwisho zilizozaa mabao na nyingine washambulizi wenzake walishindwa
kuzitumia vema.
Kunako
dakika ya 45 Munir kwa mara nyingine tena alirejea kambani akiifungia
Barcelona bao la tatu, na kufanya matokeo kuwa 3-0 hadi kumalizika kwa
kipindi cha kwanza.Kipindi cha pili Leicester City waliingia kitofauti
kabisa hasa baada ya kuingia kwa mchezaji Mussa waliyemsajili toka timu
ya CSK Moscow kwani dakika moja ya kipindi cha pili mchezaji huyo
akaipatia timu yake bao la kwanza kwa kuwafungisha tela wchezaji watatu
wa Barcelona toka katikati ya uwanja.
Dakika
ya 65 Mussa akaipatia Leicester City bao la pili kwa shuti kali ndani
ya boksi alipopata pasi toka kwa Marka aliye mnyang'anya mpira mlinzi
J.Alba, na kufanya matokeo kuwa 3-2, lakini kuna msemo usemao anaye jua
anajua tu, kwani dakika ya dakika ya 83 kinda mwingine wa Barcelona
Mujica aliipatia timu yake bao la nne baada ya walinzi wa Leicester
kuzembea kuuondo mpira kwenye eneo la hatari na kumpa mwanya mfungaji
kuutumbukiza mpira wavuni. Hadi mwisho wa mchezo huo uliopigwa huko
Stockholm Sweden,Barcelona 4 na Leicester City 2.
Nako
katika uwanja wa US Bank jimboni Minneapolis nchini Marekani, timu ya
Chelsea iliizamisha AC Milan kwa mabao 3-1 katika mchezo wa kusisimua.
Dakika ya 24 alikuwa ni mchezaji Traole aliyeanza kufungua kitabu cha
mabao kwa kufunga bao la kwanza kwa kichwa kufuatia kuuwahi mpira
uliotemwa na kipa wa Milani kutokana na shuti kali la V.Mosess.
Milan
walisawazisha bao hilo dakika ya 38 kwa mpira wa adhabu ndogo
iliyopigwa kifundi na Bonaventura na kwenda moja kwa moja wavuni.Kipindi
cha kwanza kilimalizika kwa timu hizo kuwa sare ya bao 1-1.Kipindi cha
pili mnamo dakika ya 69 Chelsea walipata penati baada ya mlinzi mmoja wa
Milan kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari na mwamuzi akaamuru ipigwe
penati,ambapo Oscar hakufanya ajizi akaiweka kambani.
Oscar
alirudi tena kimiani kuiandikia timu yake ya Chelsea bao la tatu kwenye
dakika ya 86 akiitumia pasi nzuri ya Willian.Hivyo hadi kipyenga cha
kumaliza mchezo kinapulizwa Chelsea waliibuka kidedea dhidi ya Milan kwa
mabao 3-2.
Naye
kocha Carlo Ancelotti wa Bayern Munich amedai timu yake itakuwa ya
kutisha sana na vijana wake walicheza vizuri sana licha ya kupata
kichapo cha bao 1-0 toka kwa Real Madrid. Timu hizi ziliumana vilivyo
katika uwanja wa Met Life huko Rutherford, New Jersey nchini Marekani.
Mchezo
ulikuwa wa kasi sana na wachezaji wengi vijana kuonyesha viwango vya
juu mno. Kosa kosa za hapa na pale zilitawala mchezo, Mchezaji Alaba wa
Bayern alijiona si mwenye bahati baada ya mashuti yake mawili kugonga
mtambaa panya na kutoka nje.Kipindi cha kwanza kilimalizika kwa timu
kutofungana yaani 0-0.
Kipindi
cha pili hakikuwa na mabadiliko ya kimfumo hata baada ya kila timu
kufanya mabadiliko ya wachezaji,hadi ilipofika dakika ya 78 pale
mchezaji wa Madrid Dannilo alipoipati timu yake bao pekee katika mchezo
huo.Kuingia kwa bao hilo kuliufanya mchezo kuchangamka zaidi na timu
zote kushambuliana kwa zamu lakini matokeo hayakubadilika.

Huko
nchini Uingereza timu ya Manchester United ilitoshana nguvu na timu ya
Everton kwa kutokufungana (0-0), kwenye mchezo wa hiari ulioandaliwa na
mchezaji Wayne Rooney wa Man U (W,Rooney Charity Match).
Katika
mtanange huo wa heshima kwa Rooney kuitumikia Manchester United kwa
zaidi ya miaka 10, mapato ya mchezo huo yamepelekwa kwenye vituo vinne
vy watoto ambavyo yeye amevichagua.Ndani ya dimba la Old Trafford Wayne
Rooney alipata taabu kwani mara kwa mara alikuwa akizomewa na mashabiki
wa Everton, timu ambayo aliwahi kuichezea kabla ya kujiunga na Man U.
Ibrahimovich
aliikosesha ushindi timu yake mara kadhaa hasa kwa nafasi alizo kuwa
anabaki yeye na kipa wa Everton (one against one) na mara zote hizo kipa
huyo amekuwa imara kuokoa michomo hiyo.Pia Romeo Lukaku kwa upande wa
Everton alikuwa mwiba mkali kwa walinzi wa Man U kwani aliwasumbua
vilivyo na kukosa bahati ya kufunga. Hadi mwisho matokeo yalikuwa ni
0-0.
0 comments:
Post a Comment